Pages - Menu

follow

25/08/2015

DIZASTA VINA-SIKU MBAYA

Yeah!
 Black market!
 Ringle Beatz!
VERS 1
Nakurupuka kitandani baada ya ndoto za kutisha
 Moyo unadunda sana na jasho linanitiririka
 Macho nafikicha, taswira, naona kiza
 Kwa muda nasizi kimya na dakika zinapita
Zikijirudia ndoto hatari naona woga Nakosa hoja napotafakari nilichoota Namwamsha wife
 aniwekee maji ya kuoga Ananijibu anahisi homa
 na mwili mzima umechoka Nampa pole,
 Staki kuanzisha zogo wala nini
 Maana hata sura inaonesha ana kinyongo na mimi
Ni muda sasa napokua nae hajiamini
 Nacheki saa nagundua nimechelewa kazini
Napiga zangu maji mwilini And just for the record,
 Mimi ndo mtunza funguo za ofisini Nakuta wafanyakazi na bosi wapo getini Kwa ghadhabu kila mmoja akinitazama
mimi kabla sijameza mate wala sijabuni sala Naambiwa walikuja wazabuni kwa biashara Na kwakua nilichelewa kufungua ofisi Mchongo ukafa, nimeingizia kampuni hasara Baada ya masaa kibao ya kufikiri Ofisi ikaweka kikao kunijadili Waliniona driver nimeangusha basi Wakafikia mwafaka wakunifukuza kazi Nikatahamaki,

 sikujua lakufanya Pale kwenye kamati
 hakuna wa kumtazama Nikahisi ni mipango ya kikuda imefanywa 
Sio gari tu, maana hata nyumba nilinyang'anywa
 Nikajiuliza huruma imekwenda wapi? Kila mtu alijua kua nilipenda kazi
 Niliheshimu kama navyoheshimu ndoa ama mzazi Ama muumba,
 leo nimepata doa kwenye shati Acha familia, 
vipi deni la ofisi Wamenipa mwezi, nikifeli watanifilisi 
Mtoto shule, pia bunju nina shamba la kukopa
 Sijalipa na kijiji nina ndugu wa kutosha Nguvu zilimalizika,
 nikatoka kwa adabu Licha ya ghadhabu kunishika
 Nikajipa moyo kua nna mikono pia na miguu Vyote vyangu
 sina sababu ya kushindwa Nilikosa wa kunishika 
wa kumweleza Mshahara ulikua mdogo nilishindwa kuwekeza 
Nikapiga moyo konde mimi mwanaume nita-fight 
Nikpanda gari nikampe taarifa wife Nikiwa ndani ya
dimbwi la mawazo Nikitafakari hivi vitimbi na vikwazo Mbele yangu akakatiza mpita njia Kwakua sikua makini na gari nikamvamiA
 Dakika mbili, wananchi wakalizunguka gari Wakinishutumu sana sababu ya mwendo mkali Nikaitikia wito nikitegemea thawabu Nikampeleka mgonjwa na akaanza matibabu 
Narudi zangu home, misemo ya kishenzi 
nikitema chumbani nasikia mihemo ya mapenzi
 Bila hodi, mlango nikaufungua kwa ghadhabu Nikamkuta 
house-boy juu ya kifua cha mke wangu! Nikabaki kama zuzu 
Yule wa kunifariji ndio ameniletea uchungu Nilitaka nilianzishe 
sikua na nguvu Huku nafsi inanishauri kwamba nimwachie Mungu Swalini kwamba sina moyo mkunjufu? Au kwakua muda sijaenda kuabudu? Au tuseme mja nina gundu?
 Au kwakua nilijenga nyumba na sikuwajulisha ndugu?
 Sijaona faida ya pato langu Wazazi walikufa bila kula jasho langu Mawazo kwenye kichwa yamezidi Dunia ina watu wengi na sioni \wa kunifariji Naitazama ardhi, naitazama mbingu Sioni nuru nachoona ni maumivu Maswali mengi, bila majibu Ila Swali kubwa ni vipi mimi nitaimaliza siku? Jua linazama bado sijiamini Naona nadondoka ila sioni nikifika chini Saa tano na dakika hamsini Bado dakika kumi siku iishe na sijui kinafata nini Oh my God


New video

simu tv

simu tv

MPIGIE KURA WAKAZI

MPIGIE KURA WAKAZI